1 Chronicles 1:5-23

Wana Wa Yafethi

5Wana wa Yafethi walikuwa:
Gomeri, Magogu, Madai, Yavani, Tubali, Mesheki na Tirasi.
6Wana wa Gomeri walikuwa:
Ashkenazi, Rifathi na Togarma.
7Wana wa Yavani walikuwa:
Elisha, Tarshishi, Kitimu na Rodanimu.

Wana Wa Hamu

8 aWana wa Hamu walikuwa:
Kushi, Misraimu,
Yaani Misri.
Putu na Kanaani.
9Wana wa Kushi walikuwa:
Seba, Havila, Sabta, Raama na Sabteka.
Wana wa Raama walikuwa:
Sheba na Dedani.
10 cKushi akamzaa
Nimrodi, ambaye alikua akawa mtu shujaa katika nchi.
11Misraimu akawazaa:
Waludi, Waanami, Walehabi, Wanaftuhi,
12 dWapathrusi, Wakasluhi (hao ndio asili ya Wafilisti) na Wakaftori.
13Wana wa Kanaani walikuwa:
Sidoni, mzaliwa wake wa kwanza, na Hethi,
14Wayebusi, Waamori, Wagirgashi, 15Wahivi, Waariki, Wasini, 16Waarvadi, Wasemari na Wahamathi.

Wana Wa Shemu

17 eWana wa Shemu walikuwa:
Elamu, Ashuru, Arfaksadi, Ludi na Aramu.
Wana wa Aramu walikuwa:
Usi, Huli, Getheri na Mesheki.
18Arfaksadi akamzaa Shela,
Shela akamzaa Eberi.
19Eberi alipata wana wawili:
Mmoja wao aliitwa Pelegi,
Pelegi maana yake Mgawanyiko.
kwa kuwa wakati wake dunia iligawanyika; nduguye aliitwa Yoktani.
20Wana wa Yoktani walikuwa:
Almodadi, Shelefu, Hasarmawethi, Yera,
21Hadoramu, Uzali, Dikla, 22Obali, Abimaeli, Sheba, 23Ofiri, Havila na Yobabu. Wote hawa walikuwa wana wa Yoktani.
Copyright information for SwhNEN